Mabingwa watetezi wa kombe la kagame, maarufu kama wazee wa Uturuki
leo wanatarajia kushuka dimbani kukabiliana na wakata miwa wa Manungu
Turiani Mkoani Morogoro, Mtibwa sugar, mchezo utakaopigwa uwanja wa
taifa jijini Dar es salaam. Vijana hao wa Ernie Brandts wanataraji
kuingia uwanjani kwa lengo la kuendeleza ubabe wao baada ya kutoka
nchini Uturuki kwa muda wa wiki mbili,lakini pia kulipa kisasi kwani
mzunguko wa kwanza walifungwa mabao matatu 3-0 uwanja wa jamhuri
Morogoro. | |
0 comments:
Post a Comment