Baada ya kuvuliwa ubingwa wa
michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa kutoka sare na Burkinafaso,
Zambia wanaamini bado inawezekana kwao kufuzu fainali za kombe la dunia 22014 hivyo
wachezaji wa kikosi hicho wanatakiwa kuaminiwa na kuepuka kubadilisha kikosi
hicho baada ya kutolewa hatua ya makundi ya kombe la mataifa ya Afrika AFCON.
Kocha wa Chipolopolo mfaransa,
Herve Renard amesema licha ya Zambia kutolewa hatua ya awali ya AFCON, kufuzu kombe la dunia la
mwaka 2014 nchini Brazil ndio imebaki kazi kubwa kwao.
Renard amesema Zambia walikuwa na malengo
mawili, moja ilikuwa  ni kutetea ubingwa
wao wa AFCON pili kufuzu fainali za kombe la dunia, wameshindwa la kwanza na
sasa bado wana nafsi ya kujipanga kufuzu kombe la dunia.
Kocha huyo aliongeza kuwa kuwepo
kundi moja na Ghana kuwania kufuzu kombe la dunia haitakuwa rahisi kwao lakini
watajipanga kwani walianza vizuri michezo ya kwanza.
Zambia mpaka sasa wana pointi 6
walizopata baada ya kushinda mchezo mmoja na kupewa poniti za 3 za bure kutoka kwa Sudan walioadhibiwa na FIFA kwa kosa la kumtumia mchezaji aliyesimamishwa.
Kuhusiana na kibarua chake, Renard
alisema Zambia sio kama mataifa ya mengi ya afrika ambayo hukimbilia kuwatimua makocha,
lakini Rais wa chama cha soka Zambia Kalusha Bwalya ana maarifa makubwa katika
soka, ila kama watamtaka kuondoka atakubali na wanatakiwa kukaa naye na kula
chakula cha mchana pamoja na kumwambia aende na yeye atafunga virago vyake na
kurudi nyumbani bila tatizo lolote.
Renard aliwapa Zambia ubingwa wa
kombe la mataifa mwezi februari mwaka jana bila matarajio.
Zambia hawajawahi kufuzu
fainali za kombe la dunia.
0 comments:
Post a Comment